After
all I just discovered my written Swahili isn’t that bad like the one I speak
(characterized by –di and –ndis, -chi and –shis bombarding each other unceremoniously).I
chose a simple topic to start with and the following is the importance of
tourism to Kenya according to me in Swahili.
Utalii ni hali ya kusafiri huku na huko kuyafurahia
mandhari. Pia kule kushughulikia watalii au kuwahudumia ni Utalii. Hapa nchini,
utalii huchukuliwa kama kitendo cha kusafiri mbali na mahali unakoishi, mfano
kutoka Kenya kwenda Uganda ama pia kutoka Nairobi kwenda kujivijari Nakuru. Kwa ufupi kuna viwango viwili
vya utalii; kuna kule kutembea kutoka mahali pamoja hadi pengine katika nchi
yako, almaarufu kama Domestic Tourism
kwa lugha ya kimombo na kuna kutoka nchi moja hadi nyengine.
Hapa Kenya Utalii umedhaminiwa sana kwani huchangia
pakubwa kuinua uchumi wa nchi. Mwanzo, vinavyovutia watalii hapa nchini ni
wanyama wa porini, pwani ya Kenya, vitu vya kihistoria, mila na utamaduni na
hata mazingira.
Watalii wanaotoka nchi za kigeni huleta fedha za
kigeni na hivyo kuimarisha uchumi wa nchi kwani hutumiwa kununulia vitu vingine
na kukuza maendeleo nchini. Utalii pia unasaidia kuimarisha idadi ya nafasi za
kazi za adinasi farafara nchini. Watu wanavyozidi kupata kazi ndivyo uchumi
unazidi kuimarika na umasikini kupungua.
Kupitia utalii, kuna utunzaji wa mazingira. Mjinga
pekee ndiye atakayekwambia mvua hutoka ‘mbinguni’. Miti huleta mvua. Kwa hivyo
utunzaji wa mazingira unasaidia pakubwa kuongeza idadi ya mvua katika sehemu
mbalambali nchini. Zaidi ya hayo, miti huwa chakula na mahali pakuishi pa
wanyama wengi.
Watalii wawekezaji ambao wengi wao huwa wakwasi
wenye mbango si haba, huwekeza katika sekta mbalimbali nchini. Wao hulipa
ushuru mwingi na hivyo basi kuimarisha uchumi wa nchi.
Watalii wengi huchukua ‘picha’ za wanakotembelea na
wanayoona na kisha kuwaonyesha wenzao wanaporudi nyumbani. Hii huwapa wengine
hamu ya kutembea Afrika na hapa nchini na hivyo kuongeza idadi ya watalii nchini.
Idadi ya watalii inavyoongezeka, ndivyo mapato kutokana na utalii yanavyozidi
kuongezeka.
Hata wewe unapozuru sehemu mbalimbali hapa nchini,
unajiwezesha kufahamu nchi yako vizuri. Tembelea #TEMBEA KENYA
kwenye tovuti ya Magical Kenya ujionee mengi.
To translate from Swahili to English click here
No comments:
Post a Comment